AFRIKA KUSIMAMA KWA DAKIKA 90 LEO

AFRIKA KUSIMAMA KWA DAKIKA 90 LEO

  • Michezo
  • July 26, 2025
  • No Comment
  • 53
16 / 100 SEO Score

Majira ya 5:00 usiku Afrika na Dunia nzima itasimama kwa dakika 90 pale timu ya taifa ya wanawake ya Morocco itakapokua uwanjani katika fainali ya fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) kucheza dhidi ya mabingwa wa wakati wote wa michuano hiyo, timu ya taifa ya wanawake ya Nigeria.

Historia inaonesha kuwa Nigeria hii leo inawania taji la 10 la Afrika upande wa wanawake, na wataingia katika mchezo huo wakiwa hawajafungwa mchezo wowote na wakiwa wameruhusu bao moja pekee.

 

Wakati huo Morocco wenyeji na waandaji wa mashindano ya WAFCON msimu huu wataingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu ya kutofungwa mchezo wowote lakini wakiwa wanatafta kutwaa kombe hili kwa mara ya kwanza kabisa.

Mchezo huo utachezwa katika uwanja wa Olimpiki, wenye uwezo wa kuchukua watu 21,000 uliopo katika jiji la Rabat nchini Morocco na bingwa wa michuano hiyo msimu huu akivuna kiasi cha dola za Kimarekani $1m (£743,000) pamoja na kombe jipya la WAFCON.

 

Related post

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YATINGA MANYARA NA ARUSHA

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI…

10 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Sixmund Begashe, Arusha Timu ya wataalamu wa Ufuatiliaji na Tathmini…
HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu HALMASHAURI ya Mji Handeni imeainisha mikakati mitano ya…
RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *