AHOUA ANAONGOZA MBIO ZA MFUNGAJI BORA MSIMU HUU

AHOUA ANAONGOZA MBIO ZA MFUNGAJI BORA MSIMU HUU

  • Michezo
  • May 9, 2025
  • No Comment
  • 65

Kiungo Mshambuliaji wa Simba SC, Jean Charles Ahoua amezidi kujiweka katika nafasi nzuri kuelekea katika mbio za kutwaa kiatu cha mfungaji bora wa NBC msimu huu baada ya hapo jana kufunga mabao matatu katika ushindi wa mabao 5-1 walioupata Simba dhidi ya Pamba Jiji FC.

 

Ahoua sasa amefikisha mabao 15 kwenye mbio za ufungaji bora akimshusha straika wa Yanga, Clement Mzize mwenye mabao 13, huku Prince Dube na Leonel Ateba wakiwa na mabao 12 kila mmoja.

 

MVP huyo wa msimu uliopita katika Ligi ya Ivory Coast yupo kwenye mazingira mazuri ya kushinda kiatu cha ufungaji kutokana na kuwa na faida ya mchezo mmoja mkononi.

 

Mpaka sasa vinara wa upachikaji mabao wa NBC ni hawa hapa:

 

🇨🇮 Jean Ahoua: 1️⃣5️⃣

🇹🇿 Clement Mzize: 1️⃣3️⃣

🇿🇼 Prince Dube: 1️⃣2️⃣

🇨🇲 Ateba: 1️⃣2️⃣

🇬🇭 Jonathan Sowah: 1️⃣1️⃣

🇰🇪 Elvis Rupia: 1️⃣0️⃣

Related post

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YATINGA MANYARA NA ARUSHA

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI…

10 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Sixmund Begashe, Arusha Timu ya wataalamu wa Ufuatiliaji na Tathmini…
HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu HALMASHAURI ya Mji Handeni imeainisha mikakati mitano ya…
RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *