ELON MUSK AZINDUA CHAMA KIPYA CHA KISIASA MAREKANI

ELON MUSK AZINDUA CHAMA KIPYA CHA KISIASA MAREKANI

  • Habari
  • July 6, 2025
  • No Comment
  • 47
18 / 100 SEO Score

Elon Musk, mshirika wa zamani wa Rais wa Marekani Donald Trump, jana Jumamosi alizindua chama kipya cha kisiasa nchini Marekani. Hatua hiyo inalenga kupinga kile alichokitaja kuwa “mfumo wa chama kimoja.”

Elon Musk, mfanyabiashara maarufu na mshirika wa zamani wa Rais wa Marekani Donald Trump, jana Jumamosi alizindua chama kipya cha kisiasa nchini Marekani.

Hatua hiyo inalenga kupinga kile alichokitaja kuwa “mfumo wa chama kimoja” unaodhoofisha demokrasia nchini humo.

Kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter), Musk aliandika: “Linapokuja suala la kufilisi nchi yetu kupitia ubadhirifu na ufisadi, tunaishi ndani ya mfumo wa chama kimoja  siyo demokrasia.” Bilionea huyo ametangaza kuanzisha chama kipya kiitwacho “American Party”, ambacho amesema kitaongoza juhudi za kurekebisha mfumo wa sasa wa kisiasa.Musk, ambaye ni mmoja wa watu matajiri zaidi duniani na alikuwa mfadhili mkubwa wa kampeni ya Trump kwa uchaguzi wa 2024, aliingia katika mvutano mkubwa na rais huyo, baada ya Musk kuongoza jitihada za Chama cha Republican kupunguza matumizi ya serikali na kupunguza ukubwa wa utawala wa shirikisho alipokuwa akiongoza Idara ya Ufanisi Serikalini (DOGE).

Tofauti zao zilijikita zaidi katika mpango wa matumizi makubwa ya ndani uliopendekezwa na Trump, ambao Musk aliupinga vikali. Alionya kuwa mpango huo unaweza kulipua deni la taifa, na akaahidi kutumia ushawishi wake wa kisiasa kuwazuia wabunge wanaounga mkono pendekezo hilo.

Chanzo:Dw kiswahili

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *