EWURA YAPEWA KONGOLE NA MKUU WA WILAYA  YA ILEJE KWA KUELIMISHA WADAU WA MAFUTA NA GESI

EWURA YAPEWA KONGOLE NA MKUU WA WILAYA YA ILEJE KWA KUELIMISHA WADAU WA MAFUTA NA GESI

  • Habari
  • July 12, 2025
  • No Comment
  • 54
13 / 100 SEO Score

 

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, tarehe 12 Julai 2025 imeendesha semina ya kuwajengea uelewa wadau wa mafuta na gesi ya kupikia katika Wilaya ya Ileje, mkoani Songwe. Semina hiyo iliyohusisha wajumbe wa Baraza la Biashara la Wilaya, watoa huduma wa bidhaa za mafuta na gesi na wafanyabiashara, imelenga kuhamasisha uwekezaji salama na endelevu katika sekta hiyo.

Akifungua semina hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Mhe. Farida Mgomi ameipongeza EWURA kwa kazi kubwa ya kuelimisha umma na kuitikia wito wa wilaya kuja kutoa mafunzo hayo muhimu.

“Nawapongeza sana EWURA kwa kazi nzuri wanayoifanya. Kuja kwenu Ileje ni hatua kubwa ya maendeleo kwa wananchi wetu. Mafunzo haya yataongeza uelewa kwa wawekezaji wetu wa ndani, kusaidia kupanua biashara zao kwa kufuata sheria na taratibu sahihi, na pia kuhakikisha usalama wa wananchi katika matumizi ya gesi na mafuta,” alisema Mhe. Mgomi.

Aidha, Mhe. Mgomi alieleza kuwa kupitia elimu hiyo, fursa zaidi za uwekezaji zitafunguka, huku akiahidi kuwa ofisi yake itaendelea kushirikiana na EWURA na wadau wengine katika kuboresha mazingira ya biashara wilayani humo.

Semina hii ni sehemu ya mwendelezo wa jitihada za EWURA katika kutoa elimu kwa umma na kuimarisha uelewa wa jamii kuhusu huduma za nishati.

Related post

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YATINGA MANYARA NA ARUSHA

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI…

10 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Sixmund Begashe, Arusha Timu ya wataalamu wa Ufuatiliaji na Tathmini…
HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu HALMASHAURI ya Mji Handeni imeainisha mikakati mitano ya…
RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *