HANDENI MJI YAFANYA BONANZA LA MICHEZO KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

HANDENI MJI YAFANYA BONANZA LA MICHEZO KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

  • Habari
  • October 19, 2025
  • No Comment
  • 15
15 / 100 SEO Score

HANDENI TC

Halmashauri ya Mji wa Handeni imefanya bonanza kubwa la michezo lililolenga kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Bonanza hilo limefanyika leo katika Uwanja wa Kigoda, Handeni, na limehusisha wananchi, watumishi wa umma, viongozi wa dini, viongozi wa kisiasa na taasisi binafsi.

Akizungumza katika bonanza hilo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewataka wananchi wote waliojiandikisha kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kupiga kura ili kutimiza haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka.

“Nawasihi wananchi wote wa Handeni kujitokeza mapema siku ya uchaguzi. Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa saa 1:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni. Serikali imeimarisha ulinzi na usalama, hivyo kila mmoja atapiga kura kwa amani na utulivu kama tulivyoshiriki bonanza letu leo,” amesema Mhe. Nyamwese.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Handeni, Maryam Ukwaju, amewahimiza watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla kuendeleza ushirikiano na mshikamano kupitia michezo, akibainisha kuwa michezo ni chachu ya umoja na afya bora.

Bonanza hilo lilihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, kukimbia, kuvuta kamba, na mbio za taratibu.

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *