MASHAMBULIZI YA URUSI YAUA WATU 31 UKRAINE

MASHAMBULIZI YA URUSI YAUA WATU 31 UKRAINE

  • Habari
  • August 1, 2025
  • No Comment
  • 44
14 / 100 SEO Score

Mamlaka za Ukraine zimesema Ijumaa kuwa idadi ya waliouawa mjini Kiev kufuatia shambulio la jana la Urusi, imefikia watu 31 baada ya miili zaidi kupatikana chini ya vifusi.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema kuwa mwezi uliopita wa Julai, Urusi iliishambulia Ukraine kwa kutumia droni 3,800 na karibu makombora 260.

Zelensky ametaja kuridhishwa na ukweli kwamba Marekani, mataifa ya Ulaya, na washirika wengine wanaona wazi na kulaani kile kinachotokea huku akisisitiza kuwa mashambulizi ya Urusi yanaweza kusitishwa ikiwa kutakuwepo juhudi za pamoja.

Hayo yanajiri wakati Ujerumani imesema leo kuwa itaanza hivi karibuni kuwasilisha kwa Ukraine mifumo miwili ya ulinzi wa anga ya Patriot iliyotengenezwa na Marekani.

Related post

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YATINGA MANYARA NA ARUSHA

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI…

10 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Sixmund Begashe, Arusha Timu ya wataalamu wa Ufuatiliaji na Tathmini…
HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu HALMASHAURI ya Mji Handeni imeainisha mikakati mitano ya…
RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *