MHANDISI MWAJUMA ASISITIZA UWAJIBIKAJI NA UWAZI KATIKA UTUMISHI WA UMMA

MHANDISI MWAJUMA ASISITIZA UWAJIBIKAJI NA UWAZI KATIKA UTUMISHI WA UMMA

  • Habari
  • October 27, 2025
  • No Comment
  • 21
13 / 100 SEO Score

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri, ameelekeza kazi zote katika wizara hiyo zifanyike kwa kuzingatia Sheria, Taratibu, Kanuni na Miongozo ya Utumishi wa Umma.

Amesema hayo wakati akizungumza na watumishi wa Idara ya Utawala ya Wizara ya Maji, akisisitiza umuhimu wa uadilifu na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yao.

“Ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa kila kazi inafanywa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa. Hii itasaidia kuimarisha utumishi bora na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi,” amesema Mhandisi Mwajuma.

Aidha,amesisitiza suala la kuzingatia mabadiliko yanayojitokeza katika mfumo wa utumishi wa umma na kutoa majibu kwa watumishi wanapokumbana na changamoto katika masuala mbalimbali.

“Watumishi wa umma wanapokosa kuelewa au kukabiliana na changamoto fulani, ni lazima tutoe mwongozo na msaada unaohitajika ili kazi ziendelee kwa ufanisi. Hii ni sehemu ya kuhakikisha tunatimiza malengo ya Wizara kwa ufanisi,” ameongeza.

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *