MNZAVA AWATAKA WATANZANIA KULINDA AMANI WAKATI WA UCHAGUZI

MNZAVA AWATAKA WATANZANIA KULINDA AMANI WAKATI WA UCHAGUZI

  • Habari
  • October 28, 2025
  • No Comment
  • 18
13 / 100 SEO Score

Mgombea Ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Korogwe Vijijini, Timotheo Mnzava ameongoza mamia ya wananchi wa jimbo hilo katika mkutano wa kufunga kampeni huku akiwataka Watanzania wote kuepuka vishawishi vyovyote vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani .

Akiomba kura za CCM na katika mkutano uliofanyika katika kata ya Mombo, Mnzava amewahimiza vijana na wananchi kwa ujumla waendelee kuilinda amani kwa wivu mkubwa iliyoasisiwa na viongozi wa taifa letu.

Mnzava alieleza wananchi namna ambavyo wasichezee amani mana mataifa mengine ambayo hayana amani watoto, wamama na wazee wanaishi katika mazingira hatarishi na kupoteza uhai wao.

“Amani hii inayotamkwa kwenye katiba yetu, inayotamkwa kwenye dini zetu tuifate na sote tuilinde kwa kushiriki uchaguzi kwa utulivu na amani”.

Aidha Mnzava amemuombea kura Mgombea wa Urais Dkt Samia Suluhu Hassan na wananchi wamemuahidi kumchagua kwa kura nyingi za heshima na kupita kwa kishindo.

Mnzava ameleza kuwa katika kipindi chake cha uongozi, miradi ya barabara, nishati, afya na elimu imepiga hatua kubwa, akibainisha kuwa zaidi ya asilimia 100 ya vijiji vyote 118 vya jimbo hilo sasa vimeunganishwa na umeme, huku barabara za kiuchumi zikijengwa.

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *