MTAALAMU WA LISHE HANDENI AFICHUA SIRI YA MAKUNDI SITA YA CHAKULA BORA

MTAALAMU WA LISHE HANDENI AFICHUA SIRI YA MAKUNDI SITA YA CHAKULA BORA

  • Habari
  • October 15, 2025
  • No Comment
  • 25
13 / 100 SEO Score

HANDENI-TC

Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Handeni, mkoani Tanga, Esther Herman, ametoa wito kwa wananchi kuzingatia ulaji wa chakula bora kinachojumuisha makundi sita muhimu ili kuepuka magonjwa yatokanayo na lishe duni.

Akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Chakula Duniani yanayofanyika kitaifa jijini Tanga, chini ya kaulimbiu “Tuungane pamoja kupata chakula bora kwa maisha bora ya baadaye”, Esther ametaja makundi hayo ni wanga, protini, mboga za majani, matunda, mafuta pamoja na maji.

Amesema kila kundi lina umuhimu wake mwilini, na ulaji usio sahihi unaweza kusababisha udhaifu wa kinga ya mwili, utapiamlo, au uzito uliopitiliza.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa elimu ya lishe kuanzia ngazi ya kaya, akibainisha kuwa jamii nyingi bado hazina uelewa sahihi kuhusu mlo kamili, jambo linalochangia changamoto za afya kwa watoto na watu wazima.

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *