PRESHA YAONGEZEKA KWA KOCHA MOROCCO BAADA YA STARS KUPOTEZA MECHI YA NNE MFULULIZO

PRESHA YAONGEZEKA KWA KOCHA MOROCCO BAADA YA STARS KUPOTEZA MECHI YA NNE MFULULIZO

  • Michezo
  • October 14, 2025
  • No Comment
  • 20
11 / 100 SEO Score

TIMU  ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imeendelea kupata matokeo mabaya baada ya kupoteza mchezo wake wa nne mfululizo, kufuatia kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Iran katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa leo Jumanne, Oktoba 14, mjini Dubai.

Stars, ambayo haijapata ushindi tangu ilipotolewa kwenye hatua ya robo fainali ya CHAN 2024 kwa kufungwa na Morocco bao 1-0, imekuwa ikisuasua pia katika michezo ya kufuzu Kombe la Dunia, ikipoteza mechi mbili mfululizo dhidi ya Niger na Zambia kwa matokeo kama hayo.

Matokeo haya yanazidisha presha kwa Kocha Hemed Morocco, ambaye alikabidhiwa majukumu ya kuinoa timu hiyo baada ya kuondoka kwa kocha wa zamani kutoka Algeria, Adel Amrouche, mwaka 2024.

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *