RAILA ODINGA AFARIKI DUNIA

RAILA ODINGA AFARIKI DUNIA

  • Habari
  • October 15, 2025
  • No Comment
  • 13
9 / 100 SEO Score

WAZIRI Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga, amefariki dunia leo Jumatano 15,2025 akiwa na umri wa miaka 80.

Taarifa zinaeleza kuwa kiongozi huyo wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM)amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali moja nchini India.

Kifo chake kimetokea wiki chache baada ya kuzagaa tetesi mitandaoni zilizodai kuwa alikuwa katika hali mahututi, madai ambayo familia yake ilikuwa imekanusha vikali.

Awali, kaka yake mkubwa ambaye pia ni Seneta wa Siaya, Dkt. Oburu Odinga, aliwahakikishia Wakenya kuwa Raila alikuwa anaendelea kuimarika kiafya na alikuwa akipata nafuu nchini India.

Akizungumza na vyombo vya habari, Dkt. Oburu alikanusha taarifa zilizodai kwamba Raila alikuwa katika hali mbaya, akizitaja kuwa zimezidishwa na hazikuwa sahihi.

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *