RAIS SAMIA AWAONGOZA WATANZANIA KUZINDUA DARAJA LA MAGUFULI

RAIS SAMIA AWAONGOZA WATANZANIA KUZINDUA DARAJA LA MAGUFULI

  • Habari
  • June 19, 2025
  • No Comment
  • 43

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan leo June 19, 2025 amezindua daraja la JP Magufuli maarufu Kigongo-Busisi lenye urefu wa kilomita 3 lililoigharimu serikali ya Tanzania kiasi cha shilingi bilioni mia saba na elfu kumi na nane 718 za kitanzania.

 

Ujenzi wa Daraja hilo ndani ya ziwa Victoria ulianza rasmi tarehe 25, mwezi wa pili mwaka 2020 katika eneo la Kigongo –Busisi na kuchukua miaka mitano na miezi mine hadi kukamilika kwake.

Akizindua daraja hilo Rais Samia amesema

“Daraja hili ni kielelezo kikubwa cha uwezo wetu kama taifa wa kufanya maamuzi, wa kufanya maendeleo ya kwetu sisi wenyewe. Kanda ya ziwa inakwenda kuchechemka katika uchumi wa kisasa ambao utaleta ajira kwa vijana.”

 

Daraja hili sasa litaenda kuondoa kero ya wananchi ambao iliwalazimu kutumia masaa 2-6 kuvuka eneo hilo sasa watatumia mwendo wa chini ya dakika kumi kuvuka kupitia Kigongo-Ferry. Inakadiriwa magari takribani mia nane na watu elfu 13 watavuka katika daraja hili kwa muda mfupi.

Related post

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YATINGA MANYARA NA ARUSHA

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI…

10 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Sixmund Begashe, Arusha Timu ya wataalamu wa Ufuatiliaji na Tathmini…
HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu HALMASHAURI ya Mji Handeni imeainisha mikakati mitano ya…
RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *