TLS YALAANI VITENDO VYA UDHALILISHAJI DHIDI YA LISSU

TLS YALAANI VITENDO VYA UDHALILISHAJI DHIDI YA LISSU

  • Habari
  • August 1, 2025
  • No Comment
  • 46
11 / 100 SEO Score

Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) kimelaani vitendo wanavyodai ni udhalilishaji na ukandamizaji vinavyofanywa na Jeshi la Magereza dhidi ya Mwanachama wao, Wakili Tundu Lissu wakati shauri lake likiendelea Mahakamani.

TLS imesema vitendo anavyofanyiwa vinakiuka Katiba ya Tanzania na Mikataba ya Kimataifa inayolinda haki, na utu wa kila Mtu.

 

TLS imeomba kukutana na Jaji Mkuu kujadili suala hilo na kulitaka Jeshi la Magereza kuacha mara moja vitendo hivyo, ikiwemo kuzuia askari wasiotambulika kuingia mahakamani na kuwachukulia hatua askari wote waliohusika katika shambulio dhidi ya Lissu, Julai 30, 2025.

 

Chama hicho kimesema iwapo mambo haya hayataheshimiwa, Uongozi wa TLS hautasita kuchukua hatua za dharura kulinda hadhi za Wanachama wake na Haki Jinai Nchini ili kutuma ujumbe wa wazi na thabiti dhidi ya ukiukwaji wa haki za Wakili yeyote.

Credit: Jamii Forums

 

Related post

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YATINGA MANYARA NA ARUSHA

TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA WIZARA YA MALIASILI…

10 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Sixmund Begashe, Arusha Timu ya wataalamu wa Ufuatiliaji na Tathmini…
HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

HANDENI MJI YAAINISHA MIKAKATI MITANO KUIMARISHA AFUA ZA LISHE

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu HALMASHAURI ya Mji Handeni imeainisha mikakati mitano ya…
RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *