WAHAMIAJI WASIO NA VIBALI KUPELEKWA GUANTANAMO

WAHAMIAJI WASIO NA VIBALI KUPELEKWA GUANTANAMO

  • Habari
  • January 30, 2025
  • No Comment
  • 64

Kufuatia Amri Ya Kuwaondoa Raia Wote Wanaoishi Bila Vibali, Rais Wa Marekani, Donald Trump, Ametangaza Mipango Ya Kuandaa Kituo Cha Kuwazuia Wakimbizi Hao Katika Gereza La Kijeshi La Guantanamo.

 

Vyama Vya Wafanyakazi Wa Serikali Nchini Marekani Vimewashauri Wanachama Wake Kuwa Makini Na Utawala Wa Trump Na Kupendekeza Mpango Wa Kujitolea Kujiuzulu Mpango Ambao Utawawezesha Wafanyakazi Kujiuzulu Kwa Malipo Ya Mshahara Wa Miezi Minane.

 

Wakati Huo Rais Wa Cuba, Miguel Diaz-Canel, Ameielezea Mipango Hiyo Kuwa Ya Ukatili, Akidai Kuwa Wakimbizi Hao Watawekwa Karibu Na Vituo Vilivyotumika Kwa Mateso Na Vifungo Vinavyokiuka Sheria.

 

Kituo Hicho, Ambacho Ni Tofauti Na Gereza Hilo Lenye Ulinzi Mkali, Kiliwahi Kutumika Miaka Ya Nyuma Kuhifadhi Wakimbizi, Wakiwemo Wahaiti Na Wacuba Waliokamatwa Baharini Na Kitakua Na Uwezo Wa Kupokea Wahamiaji Elfu 30.

✍️| Kastul Elias

Related post

JKT,REA WAANZISHA UBIA WA KIHISTORIA:MRADI WA BILIONI TANO WA NISHATI SAFI KAMBI ZA  JKT

JKT,REA WAANZISHA UBIA WA KIHISTORIA:MRADI WA BILIONI TANO WA…

17 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Alex Sona, Dodoma KATIKA  hatua inayoweza kuelezwa kama mpango wa…
NAIBU WAZIRI MWANAIDI AZITAKA NGOs KUWAJIBIKA NA KUTOA HUDUMA KWA UWAZI KWA WANANCHI

NAIBU WAZIRI MWANAIDI AZITAKA NGOs KUWAJIBIKA NA KUTOA HUDUMA…

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum,…
WAKULIMA WAASWA KUWEKEZA KWENYE VITUO VYA MAFUTA,BIASHARA YA LPG

WAKULIMA WAASWA KUWEKEZA KWENYE VITUO VYA MAFUTA,BIASHARA YA LPG

17 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Balozi Simon Sirro,akipata maelezo kutoka…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *