WANANCHI KUPATA VIBALI NA LESENI BILA KUFIKA OFISINI-EWURA

WANANCHI KUPATA VIBALI NA LESENI BILA KUFIKA OFISINI-EWURA

  • Habari
  • October 6, 2025
  • No Comment
  • 21
13 / 100 SEO Score

 

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile (kulia), akizungumza na watumishi wa Mamlaka hiyo wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja uliofanyika leo Oktoba 6,2025  katika ofisi za EWURA jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imerahisisha upatikanaji wa vibali, leseni na utatuzi wa malalamiko kupitia mifumo ya kidijitali, hatua inayowawezesha wananchi kupata huduma popote walipo na kwa wakati bila kulazimika kufika ofisini.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile, wakati akizindua maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa Wateja, katika ofisi za EWURA, Dodoma, leo 6.10.2025.

“Tumeendelea kuboresha mifumo yetu ya kidijiti ambayo imeimarisha utoaji wa huduma kwa kasi zaidi na kwa wakati, na kuondoa kabisa malalamiko ya ucheleweshwaji yaliyokuwepo awali” alisema Dkt.Andilile

EWURA inatumia mifumo kadhaa ya kidijiti ikiwamo E- LUC, ambao unasaidia kupokea mrejesho na maoni ya wateja juu ya namna wanavyopokea huduma zinazodhibitiwa kutoka kwa watoa huduma wanaosimamiwa na EWURA. Mfumo huu unapatikana katika aplikesheni ya simu ya kiganjani.

Pia upo mfumo wa LOIS unaorahisisha maombi ya leseni, vibali vya ujenzi wa miundombinu ya bidhaa zinazodhibitiwa pamoja na uwasilishaji wa malalamiko yanayohusu huduma za nishati na maji.

Dkt Andilile amewataka wafanyakazi wa EWURA kuendelea kutoa huduma kwa weledi na kwa wakati ili wateja wake wafurahie zaidi huduma za udhibiti.

 

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile (kulia), akizungumza na watumishi wa Mamlaka hiyo wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja uliofanyika leo Oktoba 6,2025  katika ofisi za EWURA jijini Dodoma.

Baadhi ya wafanyakazi wa EWURA wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mkurugenzi Mkuu, Dkt. James Andilile, wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja leo  Oktoba 6,2025 .

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *