WATENDAJI WAHIMIZWA KUSHIRIKIANA NA VYOMBO VYA KUDHIBITI WAHAMIAJI HARAMU

WATENDAJI WAHIMIZWA KUSHIRIKIANA NA VYOMBO VYA KUDHIBITI WAHAMIAJI HARAMU

  • Habari
  • July 27, 2025
  • No Comment
  • 37
13 / 100 SEO Score

Na Mwandishi Wetu.

Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro Kiseo Yusuph Nzowa ametoa wito kwa maafisa Tarafa na Watendanji wa Kata kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama ili kudhibiti wimbi la uhamiaji haramu katika maeneo yao ya kiutawala.

Katibu tawala Nzowa ametoa agizo hilo wakati alikihitimisha mafunzo ya siku mbili ya maafisa tarafa na watendaji wa kata wapya walioajiriwa kuanzia mwezi Julai, 2024/2025.

Amesema “Kila mtanzania ana jukumu la kuitunza amani tuliyonayo lakini nyinyi viongozi ndiyo kiungo muhimu wa mamlaka nyingine katika serikali yetu, hivyo hili la kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama ni muhimu mno katika kudumisha amani tuliyonayo kwa kudhibiti vitendo vya kihalifu ikiwa ni pamoja na kuwabaini na kuwatolea taarifa wahamiaji haramu”.

Aidha amewataka maafisa hao kulipa kipaumbele suala la ukusanyaji wa mapato ya ndani katika mamlka za serikali za mitaa, ili kuiwezesha serikali kupata nguvu za kiuchumi na kifedha kuendelea kujenga miradi mbaimbali ya maendeleo kama vile hospitali,barabara, shule, umeme na maji.

Mafunzo hayo kwa Maafisa tarafa na watendaji wa kata katika kanda ya kasikazini yamewashirikisha washiriki kutoka mikoa ya Arusha,Tanga, Kilimanjaro na Manyara.

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *