WAZIRI MKUU ASIFIA VETA KWA KUTEKELEZA DHANA YA USHIRIKISWAJI KWA VITENDO

WAZIRI MKUU ASIFIA VETA KWA KUTEKELEZA DHANA YA USHIRIKISWAJI KWA VITENDO

  • Habari
  • October 11, 2025
  • No Comment
  • 138
13 / 100 SEO Score

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameipongeza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kwa jitihada zake za kuwawezesha vijana wenye mahitaji maalum kupata ujuzi wa kazi, akisema hatua hiyo ni mfano halisi wa utekelezaji wa dhana ya ushirikishwaji kwa vitendo.

Majaliwa alitoa pongezi hizo jana tarehe 10 Oktoba, 2025 alipokuwa akitembelea banda la VETA katika maadhimisho ya Wiki ya Vijana yanayofanyika mkoani Mbeya, ambako alishuhudia vijana wenye ulemavu wakiwasilisha kazi zao katika fani mbalimbali ikiwemo ushonaji wa nguo na teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA).

Katika banda hilo, Waziri Mkuu alikutana na Francis Anthony, mhitimu wa VETA ambaye kwa sasa ni mwalimu wa kompyuta. Francis alieleza jinsi alivyopata mafunzo na baadaye kuajiriwa kufundisha vijana wengine.

“Nilianza kama mwanafunzi wa VETA, sasa ninafundisha. Hii ni ishara kuwa vijana wenye ulemavu wakipewa nafasi, wana uwezo wa kuchangia maendeleo ya taifa,” alisema Francis.

Kwa upande wake, Mwanafunzi wa VETA Songea,Riziki Ndumba, alisimulia jinsi alivyoweza kumaliza kozi ya ushonaji licha ya kuanza mafunzo bila kuwa na ujuzi wowote.

“Kwa msaada wa walimu na mazingira rafiki, nimeweza kujifunza na sasa ninaweza kujitegemea,” alisema Riziki.

Akizungumzia mipango ya taasisi hiyo, Ofisa Uhusiano wa VETA, Eimer Sarao, alisema mamlaka imejipanga kuhakikisha vijana wenye ulemavu wanapata fursa sawa za mafunzo ya ufundi ili kuondoa vikwazo vinavyosababisha utegemezi.

“Tuna walimu waliowahi kuwa wanafunzi wetu wenye ulemavu. Mfano mzuri ni mwalimu anayefundisha katika Chuo cha Mafunzo Stadi Morogoro. Hii inaonyesha kuwa ulemavu si kikwazo cha mafanikio,” alisema Sarao.

VETA inaendelea kutekeleza programu maalum zinazolenga makundi mbalimbali ya kijamii, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kujenga taifa lenye nguvu kazi jumuishi, lenye stadi na tija kwa uchumi wa sasa na ujao.

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *