YANGA YATANGAZA KUUTUMIA UWANJA WA AMAAN MAKUNDI CAFCL

YANGA YATANGAZA KUUTUMIA UWANJA WA AMAAN MAKUNDI CAFCL

  • Habari
  • November 5, 2025
  • No Comment
  • 3
9 / 100 SEO Score

KLABU ya Yanga imetangaza rasmi kwamba mechi zake za nyumbani katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu zitachezwa katika Uwanja wa New Amaan Complex uliopo Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe, amesema kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya tathmini ya kina kwa kuzingatia maslahi mapana ya klabu.

Yanga, ambayo imepangwa Kundi B pamoja   na vigogo wa Afrika Kaskazini ambazo ni Al Ahly ya Misri, JS Kabylie ya Algeria na AS FAR ya Morocco imeamua kuhamishia michezo hiyo visiwani humo, baada ya kutumia Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, katika mechi za awali dhidi ya Wiliete ya Angola na Silver Strikers kutoka Malawi.

“Baada ya kufanyika tathmini ya kina na kwa maslahi mapana ya klabu yetu, napenda kuwatangazia kwamba mechi za Yanga katika hatua ya makundi zitafanyika katika kisiwa cha Unguja kwenye Uwanja wa New Amaan Complex,” amesema Kamwe.

“Nichukue fursa hii kuwaomba mashabiki na wanachama wa Yanga katika visiwa vya Pemba na Unguja kuanza maandalizi ya haraka kuhakikisha tunafanya vizuri.”ameongeza

Wakati huo huo, ameelezwa kuwa Yanga itaendelea kutumia Uwanja wa KMC Complex kwa michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara na mashindano mengine ya ndani.

Uamuzi huo unaifanya Yanga kuwa klabu ya tatu kutoka Tanzania Bara kutumia Uwanja wa New Amaan Complex kwa mechi za mashindano ya Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) msimu huu, baada ya Singida Black Stars na Azam FC zinazoshiriki Kombe la Shirikisho Afrika.

Related post

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

RAIS SAMIA ATEUA WABUNGE SITA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO JIJINI DODOMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score MKUTANO wa kwanza wa Bunge la 13 unatarajiwa kuanza rasmi kesho,…
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

13 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *