BEI ZA MAFUTA MWEZI SEPTEMBA ZAENDELEA KUSHUKA

BEI ZA MAFUTA MWEZI SEPTEMBA ZAENDELEA KUSHUKA

  • Habari
  • September 3, 2025
  • No Comment
  • 24
12 / 100 SEO Score

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA 

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei kikomo za mafuta zinazotumika kuanzia leo Septemba 3, 2025, zikionesha kupungua kwa kwa shilingi 36 kwa bei ya petroli na shilingi 23 kwa bei ya dizeli kwa mafuta yaliyopokelewa bandari ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara mtawalia.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt James Andilile, bei ya petroli katika soko la dunia imepungua kwa asilimia 0.2 %, dizeli kwa 5.5 % na mafuta ya taa kwa 3.5%. Vilevile, kwa bei za mwezi Septemba, 2025, wastani wa gharama za kubadilisha fedha za kigeni umepungua kwa 3.96%

Gharama za kuagiza mafuta katika Bandari ya Dar es salaam zimeongezeka kwa wastani wa 20.73% kwa mafuta ya petroli, 7.75% kwa mafuta ya dizeli na 2.62% kwa mafuta ya taa; katika Bandari ya Mtwara hakuna mabadiliko, na kwa Bandari ya Tanga zimepungua kwa 12.66% kwa mafuta ya petroli na 12.66% kwa mafuta ya dizeli.

Aidha, wafanyabiashara wanakumbushwa kuuza mafuta kwa bei zilizoidhinishwa na EWURA na yeyote atakayekiuka agizo hili atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *