YANGA SC YANG’ARA UGENINI LIGI YA MABINGWA AFRIKA

YANGA SC YANG’ARA UGENINI LIGI YA MABINGWA AFRIKA

  • Michezo
  • September 19, 2025
  • No Comment
  • 25
17 / 100 SEO Score

LUANDA, ANGOLA 

MABINGWA  wa Ligi Kuu Tanzania Bara,Timu ya  Young Africans SC, imeanza vyema kampeni zao za Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuichapa Wiliete SC ya Angola mabao 3-0 katika mchezo wa awali  uliopigwa kwenye Uwanja wa Estadio 11 de Novembro, jijini Luanda.

Bao la kwanza la Yanga lilipatikana dakika ya 31 kupitia Aziz Andabwile, aliyepiga shuti kali kutoka nje ya 18 lililomshinda kipa wa Wiliete na kupelekea Wanajangwani kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa bao 1-0.

Kipindi cha pili kilishuhudia Yanga wakiongeza kasi ya mashambulizi mnao Dakika ya 72, Edmund John alifunga bao la pili kwa pasi safi ya Maxi Nzengeli, kabla ya Prince Dube kufunga la tatu dakika ya 82 akiwa ndani ya boksi baada ya kuwachambua mabeki wa  Wiliete.

 Washambuliaji wa Yanga wakikosa nafasi mbalimbali huku Dube akikosa nafasi nyingi  kabla ya kufunga bao la  tatu.

Kwa Ushindi huo  Yanga unawapa  faida kubwa kuelekea mchezo wa marudiano  unaotarajiwa kuchezwa Septemba 27,2025 katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Kwa matokeo hayo, Yanga wamejipatia kitita cha Shilingi milioni 15/- kupitia mpango wa Goli la Mama, utaratibu ulioanzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa ajili ya kuhamasisha ushindi wa timu za taifa na vilabu vinavyoshiriki michuano ya kimataifa.

Dkt. Samia amekuwa kinara wa kusapoti michezo nchini kupitia motisha mbalimbali ambazo zimezidi kuinua ari ya wachezaji na vilabu kushindana kwa ufanisi zaidi kimataifa.

Kesho Timu ya Simba SC itashuka ugenini kucheza  dhidi ya Gaborone United nchini Botswana Kombe la Ligi ya Mabingwa Afrika huku Azam FC itakuwa ugenini  jijini Juba nchini Sudan Kusini, kukipiga na El Merriekh Bentui na Mabingwa wa Kombe la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) Singida BS watakuwa nchini Rwanda katika dimba la Pele kuwakabil Rayon Sports. 

Related post

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…
TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *