VIFAA VYA KISASA VYA MAFUNZO VYAMVUTIA PROF.NOMBO KATIKA KITUO CHA  MUHAS

VIFAA VYA KISASA VYA MAFUNZO VYAMVUTIA PROF.NOMBO KATIKA KITUO CHA  MUHAS

  • Habari
  • September 22, 2025
  • No Comment
  • 21
13 / 100 SEO Score

 

Na.Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amesema kuwa utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Kituo cha Umahiri cha Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) utakuwa chachu ya kukuza ujuzi wa wataalamu wa afya nchini.

Prof. Nombo alitoa kauli hiyo Septemba 2025 Jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa kikao cha kwanza cha Kamati ya Uendeshaji ya mradi huo, kilichofanyika katika Kituo cha Umahiri kilichopo Mloganzila. Alieleza kuwa mradi huo ni ushahidi wa wazi wa namna Serikali inavyowekeza katika kuimarisha elimu ya afya na kuhakikisha taifa linapata wataalamu mahiri wa kutoa huduma bora kwa wananchi.

“MUHAS ni taasisi inayotoa utaalamu wa kisayansi na kuandaa wataalamu wa afya kwa kiwango cha juu. Kituo hiki ni mahali pa kufundisha mabingwa na bobezi katika sayansi ya moyo na mishipa ya damu. Tunaona vifaa vinavyotumika ni vya kisasa, hivyo tunatarajia wananchi kunufaika kwa kiwango kikubwa kupitia huduma zitakazotolewa hapa,” alisema Prof. Nombo.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Prof. Appolinary Kamuhabwa, ameishukuru Serikali kwa uwekezaji mkubwa katika Kituo cha Umahiri cha Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu kilichopo Mloganzila, pamoja na ushirikiano wa kimataifa uliowezesha chuo hicho kupata ufadhili wa vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia.

Prof. Kamuhabwa amesema kuwa mchango wa Serikali na wadau wa maendeleo kutoka mataifa mbalimbali umeimarisha uwezo wa MUHAS katika kutoa mafunzo ya kibingwa na kuendeleza tafiti za kisayansi.

Mradi huo unatarajiwa kuongeza uwezo wa kitaalamu wa MUHAS katika kutoa mafunzo ya vitendo na huduma za kibingwa, sambamba na kuimarisha miundombinu ya kisasa kwa ajili ya tafiti na mafunzo ya afya ya moyo na mishipa ya damu.

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *