YANGA SC YAICHAPA PAMBA JIJI MCHEZO WA LIGI KUU TANZANIA BARA

YANGA SC YAICHAPA PAMBA JIJI MCHEZO WA LIGI KUU TANZANIA BARA

  • Michezo
  • September 24, 2025
  • No Comment
  • 23
9 / 100 SEO Score

Na.Alex Sonna

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga SC, wameanza kampeni za kutetea ubingwa wao kwa kishindo baada ya kuichapa Pamba Jiji ya Mwanza mabao 3-0, mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa Yanga kuongoza bao 1-0, lililofungwa na kiungo mshambuliaji Lassine Kouma dakika ya 45+4 kwa kichwa, akimalizia kona iliyochongwa na Edmund John.

Baada ya mapumziko, kocha wa Yanga alifanya mabadiliko yaliyoongeza uhai kwenye safu ya ushambuliaji na dakika ya 63 Max Nzegeli akaongeza bao la pili, akimalizia pasi safi ya Mohamed Hussein ‘Tshabalala’.

Kiungo Mshambuliaji Mudathir Yahya aliihakikishia Yanga pointi tatu muhimu baada ya kufunga bao la tatu dakika ya 90+2 kwa pasi ya Pacome Zouzoua.

Ligi hiyo itaendelea kesho ambapo wekundu wa Msimbazi, Simba SC, watakuwa wenyeji wa Fountain Gate ya Manyara kwenye uwanja huo wa Benjamin Mkapa.

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *