DKT. BITEKO AMPA POLE RAIS MWINYI, ASHIRIKI MAZISHI YA KAKA YAKE

DKT. BITEKO AMPA POLE RAIS MWINYI, ASHIRIKI MAZISHI YA KAKA YAKE

  • Habari
  • September 26, 2025
  • No Comment
  • 13
19 / 100 SEO Score

Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameungana na mamia ya waombolezaji kutoa pole kwa familia ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kufuatia kifo cha kaka yake Abass Mwinyi ambaye pia alikuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Fuoni kilichotokea Zanzibar, Unguja usiku wa kuamkia Septemba 25, 2025.

Dkt. Biteko ameshiriki mazishi hayo Septemba 26, 2025 Bumbubwini Mangapwani, Zanzibar.

Ambapo ameungana na viongozi mbalimbali akiwemo Mgombea Mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Ndugu Stephen Wasira, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla .

Aidha, baada ya mazishi baadhi viongozi walipata fursa ya kutoa heshima katika kaburi la Hayati Ali Hassan mwinyi lililopo Bumbubwini Mangapwani, Zanzibar.

Awali, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alifika msibani kuwafariji wafiwa na kisha kusaini kitabu cha maombolezo.






Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *