WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

  • Habari
  • October 22, 2025
  • No Comment
  • 7
18 / 100 SEO Score

 

Na Augusta Njoji, Handeni TC

Makundi mbalimbali ya wananchi katika Halmashauri ya Mji wa Handeni yameeleza namna yalivyojipanga kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, wakisisitiza umuhimu wa kutumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi wanaowataka.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wafanyabiashara, wajasiriamali, na wananchi wamesema wamejipanga mapema kuhakikisha wanajitokeza kupiga kura asubuhi ili kuepuka msongamano na kuhakikisha sauti zao zinasikika kupitia sanduku la kura.

Mmoja wa wajasiriamali katika Soko la Kidereko, Hadija Saidi amesema anahamasisha wenzake kupigakura mapema kwa amani na kuendelea na shughuli zao.

Kwa upande wake, Charles Mkomwa, Mfanyabiashara kata ya Kidereko, amesema uchaguzi ni fursa muhimu kwa watanzania kuchagua viongozi watakaosikiliza sauti zao.

Naye, Mwenyekiti wa Kikundi Kinamoto cha utengenezaji samani, Maulid Gumbo, amesema ana kila sababu za kujitokeza kupiga kura Oktoba 29, 2025 ili kuchagua viongozi watakaoendelea kuchochea maendeleo ya wananchi.

Related post

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera,akizungumza…
RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA HASARA

RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA…

11 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Bw. Missaile Musa amesema mafunzo yanayotolewa…
BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *