AFISA MTENDAJI WA KATA YA LIONJA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA MAKOSA YA RUSHWA.

AFISA MTENDAJI WA KATA YA LIONJA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA MAKOSA YA RUSHWA.

  • Habari
  • September 21, 2025
  • No Comment
  • 17
12 / 100 SEO Score

NA MWANDISHI WETU _ LINDI

Mnamo Septemba 18, 2025 katika mahakama ya wilaya ya Nachingwea limefunguliwa shauri la Uhujumu Uchumi namba 22689/2025 mbele ya Hakimu Mwandamizi Mkuu Mh.J.Mnguto, Jamhuri dhidi Seleman Ajibu Chimogo ambaye ni Afisa Mtendaji wa Kata ya Lionja halmashauri ya wilaya ya Nachingwea.

Mshitakiwa amefikishwa mahakamani kwa mashitaka ya Uchepuzi kinyume na kifungu cha 29 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329, marejeo ya mwaka 2023 ikisomwa pamoja na Aya ya 21,Jedwali la kwanza na kifungu cha 57(1) na 60(2)cha Sheria ya Uhujumu Uchumi Sura ya 200 marejeo ya mwaka 2023.

Mshitakiwa akiwa Afisa Mtendaji wa Kata ya Lionja ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea kwa makusudi alichepusha tani tano (5) za shehena ya mahindi ya bei nafuu (Tshs 700 kwa kilo) mali ya Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (NFRA) na kumuuzia Mfanyabiara kinyume na utaratibu. Walengwa wa mahindi hayo walikuwa ni wananchi wa kawaida kwa matumizi ya chakula na si bihashara.

Mshitakiwa amekana shitaka na yupo nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana. Shauri hilo linakuja tena Oktoba 09, 2025.

Shauri hili limefunguliwa na Mwendesha Mashitaka wa TAKUKURU Lindi Bw. Amandusy Mapunda.

TAKUKURU Lindi, Septemba 20, 2025.

Related post

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera,akizungumza…
RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA HASARA

RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA…

11 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Bw. Missaile Musa amesema mafunzo yanayotolewa…
BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *