DC MAYANJA:TANZANIA ITAJENGWA NA WATANZANIA WENYEWE

DC MAYANJA:TANZANIA ITAJENGWA NA WATANZANIA WENYEWE

  • Habari
  • September 26, 2025
  • No Comment
  • 24
13 / 100 SEO Score

 

Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja,akizungumza leo Septemba  26.09.2025 na timu ya maafisa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) walipofika ofisini kwake kwa ajili ya kujitambulisha na kumtaarifu juu ya zoezi la kampeni ya elimu ya kodi mlango mlango wilayani humo.

Na.Yahya Saleh-Chamwino

“Hatuna nchi nyingine zaidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na nchi hii itajengwa na Watanzania wenyewe.”

Ni kauli ya Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma Mhe. Janeth Mayanja wakati akizungumza leo Ijumaa tarehe 26.09.2025 na timu ya maafisa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) walipofika ofisini kwake kwa ajili ya kujitambulisha na kumtaarifu juu ya zoezi la kampeni ya elimu ya kodi mlango mlango wilayani humo.

Mhe. Mayanja amesema kuwa, nchi inajengwa kutokana na kodi zinazolipwa na wananchi.

“Miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa hapa nchini, inatokana na kodi za watanzania hivyo ni wajibu wa kila mtu mwenye vigezo vya kulipa kodi, alipe kodi kwa wakati,” alieleza Mhe. Mayanja.

Aidha, ameipongeza TRA kwa kuendelea kukusanya kodi kwa weledi na kuvuka malengo ya makusanyo huku akiisisitiza TRA kuhakikisha kila kodi inayotakiwa kukusanywa ikusanywe kwa Maendeleo ya Taifa.

“Naomba muendelee kuongeza juhudi katika ukusanyaji wa mapato na mjitahidi kuwafikia walipakodi walioko kwenye kata na vijiji mbalimbali ili sote kwa pamoja tuchangie maendeleo ya nchi yetu,” alisistiza Mkuu huyo wa Wilaya.

Naye Meneja wa TRA Wilayani Chamwino Bi. Ester Mallya amesema kuwa, kwa sasa wamejipanga kuongeza ushirikiano baina yao na Watendaji wa Kata na Wenyeviti wa Mitaa ili kuhakikisha elimu ya kodi inawafikia watu wote pamoja na kuwasajili wale wanaostahili kusajiliwa.

Related post

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera,akizungumza…
RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA HASARA

RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA…

11 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Bw. Missaile Musa amesema mafunzo yanayotolewa…
BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *