DK.NCHIMBI APOKEA BARUA YA MKAZI WA BUKOBA MJINI MWENYE ULEMAVU WA MIGUU.

DK.NCHIMBI APOKEA BARUA YA MKAZI WA BUKOBA MJINI MWENYE ULEMAVU WA MIGUU.

  • Habari
  • September 7, 2025
  • No Comment
  • 27
12 / 100 SEO Score

Mgombea mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akimsikiliza Mlemavu wa Miguu,Amos Kalungula mara baada ya kuwahutibia Wananchi wa Bukoba Mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya Msingi Kashai, leo Jumapili Septemba 7, 2025 mkoani Kagera.

….

MGOMBEA mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akimsikiliza Mlemavu wa Miguu,Amos Kalungula.

Dk.Nchimbi yuko mkoani Kagera ambako amewasili tangu jana na leo Septemba 7 ameendelea na mikutano ya kampeni ya kuomba kura za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29,2025.

Akiwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kashai Bukoba Mjini baada ya kuwahutubia wananchi,alimfuata Kalungula ambaye ni mlemavu wa miguu aliyekuwa ameshika bahasha yenye rangi ya kaki na kisha kumkabidhi Dk.Nchimbi.

Hata hivyo bahasha hiyo aliyokabidhiwa Dk.Nchimbi haijafahamika ilikuwa imebeba ujumbe gani .Hata hivyo mkazi huyo alionekana kufurahishwa na upendo ulioneshwa na Dk.Nchimbi aliyeamua kumfuata kumsikiliza na kupokea barua hiyo.

Related post

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…
TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *