DKT. KIMAMBO AWATAKA WATAALAM WA AFYA MUHIMBILI KUFUATA MIONGOZO YA KITAIFA NA KIMATAIFA KATIKA UTOAJI HUDUMA ZA DAMU

DKT. KIMAMBO AWATAKA WATAALAM WA AFYA MUHIMBILI KUFUATA MIONGOZO YA KITAIFA NA KIMATAIFA KATIKA UTOAJI HUDUMA ZA DAMU

  • Habari
  • August 18, 2025
  • No Comment
  • 32
10 / 100 SEO Score
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Dkt. Delilah Kimambo amewataka wataalam wa afya kuendelea kufuatilia miongozo ya kitaifa na kimataifa katika utoaji wa huduma za damu ili kupunguza hatari zinazoweza kujitokeza kwa wagonjwa wanaofika Hospitalini hapo.
Akizungumza hii leo Jijini Dar es Salaam kwenye ufunguzi wa mafunzo yanayolenga kujadili na kuelewa madhara yanayoweza kujitokeza kwa wagonjwa wanaoongezewa damu, amesema ni wajibu wa Madaktari, Wauguzi na Wataalam wa Maabara kuijua miongozo ya kitaifa na kimataifa ili kupunguza madhara kwa wagonjwa wanaofika kupatiwa matibabu.
“Ni lazima tuendelee kufuatilia miongozo ya Kitaifa na kimataifa katika utoaji wa huduma za damu, kwa kufanya hivyo itasaidia kwa kiasi kikubwa hatari zinazoweza kujitokeza kwa wagonjwa wetu na kuleta sifa mbaya kwetu”, amesema Dkt. Kimambo.
Aidha Dkt. Kimambo amesema matibabu ya damu ni huduma muhimu katika tiba ya magonjwa mbalimbali ikiwemo “magonjwa ya ndani, upasuaji, uzazi salama na saratani”, licha ya mchango mkubwa wa huduma hii katika kuokoa maisha lakini yapo madhara yanayoweza kumpata mgonjwa wakati au baada ya kuongezewa damu.
Hospitali ya Taifa Muhimbili hupokea maombi ya mifuko 120 hadi 150 ya damu kila siku.

Related post

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…
TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *