DKT.NCHIMBI ATUA RASMI SONGEA KUSAKA KURA ZA CCM

DKT.NCHIMBI ATUA RASMI SONGEA KUSAKA KURA ZA CCM

  • Habari
  • September 19, 2025
  • No Comment
  • 18
13 / 100 SEO Score

Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dk Emmanuel Nchimbi amewasili Songea, mkoani Ruvuma leo Septemba 19, 2025.

Dk Nchimbi ataungana tena na Mgombea urais wa chama hicho, Dkt.Samia Suluhu Hassan anayetarajiwa kuwasili kesho ambapo watakutana mkoa mmoja tangu Agosti 28, mwaka huu walipozindua kampeni za chama hicho kitaifa mkoani Dar es Salaam.

Baada ya uzinduzi,Dkt. Samia na Dk Nchimbi waligawana maeneo kwenda kunadi Ilani ya CCM na kueleza kile walichokifanya miaka mitano iliyopita na wanachotarajia kukifanya endapo watachaguliwa.

Baada ya uzinduzi, Samia yeye alianzia Morogoro, Dodoma, Songwe, Mbeya, Njombe, Iringa, Singida, Tabora, Kigoma na mikoa mitatu kati ya mitano ya Zanzibar ambayo ni, Kusini Unguja, Kaskazini Unguja na Kusini Pemba.

Dk Nchimbi yeye alianza kwa watani zake kanda ya ziwa mikoa wa Mwanza, Mara, Simiyu, Shinyanga, Geita, Kagera, Rukwa, Katavi, Arusha, Kilimanjaro, Tanga na sasa anaingia nyumbani mkoani Ruvuma.

Related post

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…
TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *