SERIKALI YAENDELEA KUIMARISHA HUDUMA ZA USTAWI KWA WAZEE.

SERIKALI YAENDELEA KUIMARISHA HUDUMA ZA USTAWI KWA WAZEE.

  • Habari
  • October 15, 2025
  • No Comment
  • 8
13 / 100 SEO Score

Na Jackline Minja – WMJJWM
Dar Es Salaam.

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kudumisha huduma bora kwa wazee kwa kuhakikisha kundi hilo linapata huduma za msingi zinazowawezesha kuishi maisha yenye heshima na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu tarehe 15 Oktoba, 2025 wakati wa ziara yake katika Makazi ya Wazee Wasiojiweza cha Tushikamane Pamoja Foundation yaliyopo Kata ya Kwembe, Manispaa ya Ubungo mkoani Dar Es Salaam.

Dkt. Jingu amesema wazee ni sehemu ya taifa kwakua wamelitumikia kwa muda mrefu kwa uaminifu na kujitolea hivyo jamii ya Watanzania wana wanawajibu wa kuwasaidia na kuwaenzi wazee kama ishara ya kuthamini mchango wao kwa maendeleo ya nchi.

“Lengo la kuwatembelea ni kuwaona kuwajulia hali na kuendelea kuwaenzi pamoja na kuthamini mchango wenu mkubwa katika kujenga na kuimarisha jamii yetu ya Tanzania, ninatambua kazi nzuri inayofanywa hapa katika kutoa huduma bora, upendo na matunzo kwa Wazee wetu.” amesema Dkt. Jingu

Aidha amewapongeza wamiliki na waendeshaji wa makazi hayo kwa moyo wa kujitolea wanaouonesha vilevile amewapongeza Manispaa ya Ubungo kwa usimamizi na uratibu wa Makazi hayo jambo linaloonesha dhamira njema ya kuhakikisha wazee wanaishi katika mazingira salama.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti Msaidizi wa Makazi ya Wazee Tushikamane Pamoja Foundation Sada Jaha amesema changamoto kubwa katika Makazi hayo ni uhaba wa watumishi ambao wanawahudumia wazee hao na amewaomba wadau na Mashirika mbalimbali kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwaenzi na kuwatunza wazee hao.

“Tunamshukuru sana Katibu Mkuu kwa kuja kutusikiliza na kutuahidi na kutuhakikishia kuwa changamoto tulizonazo zitapatiwa ufumbuzi kwa kuwa Serikali hii ni sikivu na inawajali na kuwapa kipaumbele suala la ustawi kwa wazee.” amesisitiza Sada

Nao baadhi ya Wazee waliopo katika Makazi hayo wameishukuru Serikali kwa kuwakumbuka na kuwatembelea kambini hapo ambapo kitendo hicho kinazidi kuwapa faraja na matumaini ya kuendelea kuishi na kujiona na umuhimu kama watu wengine.

Related post

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera,akizungumza…
RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA HASARA

RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA…

11 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Bw. Missaile Musa amesema mafunzo yanayotolewa…
BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *