
SERIKALI YAHIMIZA UTUNZAJI WA FEDHA VIJIJINI
- Habari
- January 23, 2025
- No Comment
- 72
Serikali Kupitia Wizara Ya Fedha, Imebainisha Kuwa Itaendelea Na Utoaji Wa Elimu Ya Fedha Na Kuhamasisha Utumiaji Wa Huduma Za Fedha Vijijini Ili Kuwawezesha Wananchi Katika Maeneo Ya Vijijini Kuwa Na Uelewa Wa Elimu Ya Fedha Pamoja Na Kuwa Na Matumizi Sahihi Ya Fedha Na Kuweka Akiba.
Hayo Yamebainishwa Na Afisa Usimamizi Wa Fedha Kutoka Idara Ya Uendelezaji Sekta Ya Fedha, Wizara Ya Fedha, Bw. Stanley Kibakaya, Wakati Timu Ya Wataalamu Kutoka Wizara Ya Fedha, Iliyoambatana Na Maafisa Kutoka Taasisi Na Wadau Mbalimbali Ilipowasili Kwa Ajili Ya Kutoa Elimu Ya Fedha Kwa Wakulima, Waendesha Bodaboda Na Wafugaji, Katika Ukumbi Wa Mikutano Wa Tarafa Ya Endabash, Wilaya Ya Karatu, Mkoani Arusha.
Bw. Kibakaya Amefanua Kuwa Elimu Hiyo Ya Fedha Italeta Mabadiliko Kwa Wananchi Hasa Ikizingatiwa Kuwa Njia Ya Uwasilishaji Kwa Filamu Itabaki Kuwa Kumbukumbu Ya Muda Mrefu Hivyo Kuendelea Kujenga Mabadiliko Ya Usimamizi Wa Fedha Binafsi.
