SGR INAVYOOKOA GHARAMA NA MUDA KWA WASAFIRI

SGR INAVYOOKOA GHARAMA NA MUDA KWA WASAFIRI

  • Habari
  • March 23, 2025
  • No Comment
  • 63

Reli ya Mwendokasi SGR  imewezesha wananchi kupata huduma ya usafiri na usafirishaji wenye Staha na gharama nafuu ambazo kila mwananchi anazimudu.

 

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dodoma, kuhusu mafanikio yanayotokana na uwekezaji wa Serikali katika reli kwa kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa amesema moja ya faida za SGR ni kupunguza muda wa safari kutoka Dar – Dodoma ni masaa 3 – 4 ikilinganishwa na masaa 9 – 12 kwa mabasi.

 

“Uendeshaji wa Reli ya SGR bila ruzuku ya Serikali, kuchochea ukuaji wa sekta nyingine za kiuchumi, upatikanaji wa ajira kwa Watanzania ambapo ajira zaidi ya 30,176 za moja kwa moja na ajira zaidi ya 150,880 zisizo za moja kwa moja zimezalishwa kupitia miradi hii, utunzaji wa mazingira ambapo takribani tani 14,327.3 za hewa ya ukaa (CO2) zimepungua, kusafirisha mzigo mkubwa kwa mara moja,” alisisitiza Masanja

 

Aidha, Kadogosa amesema kuanza huduma za usafirishaji wa kwa treni za mizigo kutaongeza uwezo wa usafirishaji  ambapo treni moja itabeba kiasi cha tani 3,000 kwa wakati mmoja, hii itapelekea kupungua kwa gharama za usafiri na hivyo kupungua kwa bei za bidhaa sokoni na kupunguza matumizi ya fedha za kigeni.

 

Akitolea mfano mafankio mengine amesema ni kusafirisha  abiria milioni 2.1 tangu kuanza kwa shughuli za usafirishaji.

 

Sanjari na hayo, SGR imewezesha kupungua kwa gharama za matengenezo ya barabara kutokana na mzigo mkubwa kusafirishwa kwa njia ya reli, kuchangia ufanisi wa bandari na ukuaji wa sekta zingine ikiwemo nishati, kilimo na viwanda, na kuchagiza ukuaji wa miji katika maeneo yaliyopo katika ushoroba wa reli.

Related post

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita…
DC NYAMWESE: MIL. 530/- KUJENGA WODI MPYA YA WAZAZI HOSPITALI YA HANDENI MJI

DC NYAMWESE: MIL. 530/- KUJENGA WODI MPYA YA WAZAZI…

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score ‎ ‎Na Job Karongo, Handeni TC ‎Mkuu wa Wilaya ya Handeni,…
WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *