UMOJA WA VINYOZI KAHAMA WAADHIMISHA SIKU YA KINYOZI DUNIANI KWA MATEMBEZI YA HISANI

UMOJA WA VINYOZI KAHAMA WAADHIMISHA SIKU YA KINYOZI DUNIANI KWA MATEMBEZI YA HISANI

  • Habari
  • September 16, 2025
  • No Comment
  • 24
16 / 100 SEO Score
Ikiwa leo dunia inaadhimisha siku ya vinyozi watoa huduma katika Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga wameiadhimisha kwa kufanya matembezi ya hisani pamoja na usafi katika Hospitali ya Manispaa ya Kahama.
 
Akizungumza baada ya zoezi hilo Mwanasheria wa Manispaa hiyo Steven Magala kwa niaba ya mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Frank Nkinda amesema Serikali inatambua mchango wa sekta hiyo muhimu ambayo inayotoa ajira kwa vijana huku akiwataka watoa huduma hao kupitia umoja wao kuendelea kushirikiana kwani Serikali ipo nao bega kwa bega.
Kwa Upande wake Katibu wa umoja wa vinyozi Wilaya ya Kahama Juma Diwani amesema maadhimisho haypo yalianza na matembezi ya amani kama sehemu ya kufikisha ujumbe kwa jamii kuhusu kada hiyo sambamba na kufanya usafi kama sehemu ya kudumisha usafi.
 
Maadhimisho ya siku ya Kinyozi duniani hufanyika kila mwaka ifikapo Septemba 16 ambapo kwa upande wa Wilaya ya Kahama yameongozwa na kauli mbiu isemayo, ‘Sekta ya vinyozi ni injini ya ajira kwa vijana, shiriki Uchaguzi mkuu’.

Related post

RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA HASARA

RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA…

11 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Bw. Missaile Musa amesema mafunzo yanayotolewa…
BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita…
DC NYAMWESE: MIL. 530/- KUJENGA WODI MPYA YA WAZAZI HOSPITALI YA HANDENI MJI

DC NYAMWESE: MIL. 530/- KUJENGA WODI MPYA YA WAZAZI…

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score ‎ ‎Na Job Karongo, Handeni TC ‎Mkuu wa Wilaya ya Handeni,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *