WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

  • Habari
  • October 22, 2025
  • No Comment
  • 6
18 / 100 SEO Score

 

Na Augusta Njoji, Handeni TC

Makundi mbalimbali ya wananchi katika Halmashauri ya Mji wa Handeni yameeleza namna yalivyojipanga kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, wakisisitiza umuhimu wa kutumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi wanaowataka.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wafanyabiashara, wajasiriamali, na wananchi wamesema wamejipanga mapema kuhakikisha wanajitokeza kupiga kura asubuhi ili kuepuka msongamano na kuhakikisha sauti zao zinasikika kupitia sanduku la kura.

Mmoja wa wajasiriamali katika Soko la Kidereko, Hadija Saidi amesema anahamasisha wenzake kupigakura mapema kwa amani na kuendelea na shughuli zao.

Kwa upande wake, Charles Mkomwa, Mfanyabiashara kata ya Kidereko, amesema uchaguzi ni fursa muhimu kwa watanzania kuchagua viongozi watakaosikiliza sauti zao.

Naye, Mwenyekiti wa Kikundi Kinamoto cha utengenezaji samani, Maulid Gumbo, amesema ana kila sababu za kujitokeza kupiga kura Oktoba 29, 2025 ili kuchagua viongozi watakaoendelea kuchochea maendeleo ya wananchi.

Related post

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…
TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *