WAFUASI WA CCM WAJITOKEZA KWA WINGI KUMSUBIRI DKT.SAMIA NA DKT.NCHIMBI INEC

WAFUASI WA CCM WAJITOKEZA KWA WINGI KUMSUBIRI DKT.SAMIA NA DKT.NCHIMBI INEC

17 / 100 SEO Score

Na .Alex Sonna-Dodoma

WAFUASI na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamejitokeza kwa wingi leo nje ya Jengo la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) jijini Dodoma, wakimsubiri kwa hamu Mgombea Urais wa chama hicho, ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Samia anatarajiwa kuwasili katika jengo hilo akiongozana na Mgombea Mwenza, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, kwa ajili ya kuchukua fomu ya uteuzi wa kugombea nafasi ya Urais kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Wafuasi hao wameonekana wakiwa na mavazi ya chama, mabango, bendera pamoja na nyimbo za kuhamasisha, ikiwa ni ishara ya kuonyesha mshikamano na kumuunga mkono mgombea wao.

Zoezi la uchukuaji fomu linafanyika kwa mujibu wa ratiba rasmi ya Tume ya Uchaguzi, ambapo vyama mbalimbali vya siasa vinawasilisha majina ya wagombea wao kwa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Related post

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera,akizungumza…
RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA HASARA

RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA…

11 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Bw. Missaile Musa amesema mafunzo yanayotolewa…
BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *