WATU SABA WAPOTEZA MAISHA MLIPUKO WA BOMU SUDAN

WATU SABA WAPOTEZA MAISHA MLIPUKO WA BOMU SUDAN

  • Habari
  • May 4, 2025
  • No Comment
  • 65

Watu wasiopungua saba wameuawa na wengine 20 wajeruhiwa kufuatia mashambulizi ya mabomu katika mji wa Old Fangak, nchini Sudan Kusini.

 

Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limethibitisha kuwa Katika mashambulizi hayo, hospitali na duka la dawa la MSF  vilivyokuwa vituo pekee vya huduma za afya katika Kaunti ya Fangak vimeharibiwa kabisa.

 

Kwa mujibu wa MSF, bomu la kwanza lilidondoshwa moja kwa moja kwenye duka la dawa na kuliteketeza kwa moto, likisababisha  uharibifu mkubwa kwa hospitali jirani.

 

Video iliyopatikana kutoka kwa mashahidi wa tukio hilo inaonyesha wakaazi wa eneo hilo wakikimbilia eneo la tukio wakiwa na ndoo za maji wakijaribu kuzima moto katika duka la dawa la MSF

Related post

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…
TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *