WAZIRI KOMBO AKUTANA NA WABUNGE MARAFIKI WA AFRIKA WA BUNGE LA JAPAN

WAZIRI KOMBO AKUTANA NA WABUNGE MARAFIKI WA AFRIKA WA BUNGE LA JAPAN

  • Habari
  • August 24, 2025
  • No Comment
  • 27
13 / 100 SEO Score

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wabunge Marafiki wa Umoja wa Afrika katika Bunge la Japan, Mhe. Yamagiwa Daishiro (Mb) tarehe 21 Agosti 2025 pembezoni mwa Mkutano wa TICAD 9 jijini Yokohama. 

Mheshimiwa Waziri Kombo na Mheshimiwa Yamagiwa pamoja na wabunge wa jumuiya hiyo wamekubaliana kuimarisha ushirikiano wa Tanzania na Japan katika sekta za teknolojia ili kuleta mabadiliko ya kidijitali; afya; jumuiya za kimataifa kwenye ajenda zenye manufaa kwa pande zote mbili; uendelezaji rasilimali watu; utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo nchini Tanzania kwa mfumo wa ubia wa sekta za umma na binafsi. 

Vilevile, walijadili umuhimu wa Japan na Tanzania kushirikiana katika usalama wa chakula hususan kwenye kuongeza uzalishaji, uhifadhi wa mazao na kutafuta masoko ya mazao ya kilimo.

Tanzania itashiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo cha Bustani yajulikanayo kama International Horticulture Expo au Green Expo ambayo yatafanyika mwaka 2027 jijini Yokohama. Maonesho hayo yatatoa fursa kwa wakulima na wafanyabiashara wa mazao ya bustani kushirikiana katika teknolojia ya kuzalisha mazao hayo na kupata masoko ya mazao hayo kwa Japan na nchi nyingine duniani ambazo zinaendelea na maandalizi ya ushiriki wa Maonesho hayo.

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *