SON ATANGAZA KUONDOKA TOTTENHAM HOTSPUR

SON ATANGAZA KUONDOKA TOTTENHAM HOTSPUR

  • Michezo
  • August 2, 2025
  • No Comment
  • 54
13 / 100 SEO Score

Baada ya kuhudumu kwa miaka 10, Nahodha wa Tottenham Son Heung-min amesema kuwa ataondoka katika klabu hiyo majira haya ya joto.

 

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Korea Kusini alijiunga na Spurs akitokea Bayer Leverkusen mwaka 2015 na amefunga mabao 173 katika mechi 454.

 

Son mwenye umri wa miaka 33, ambaye yuko chini ya mkataba na Spurs hadi 2026, yuko kwenye mazungumzo na Klabu ya Los Angeles inayoshiriki Ligi Kuu nchini Marekani.

 

Son ameelezea uamuzi huo kama uamuzi mgumu zaidi ambao ameufanya katika maisha yake ya soka.

“Nilikuja London kaskazini nikiwa mtoto, nikiwa na umri mdogo sana, mvulana mdogo alikuja London ambaye hata hakuzungumza Kiingereza, Kuondoka kwenye klabu hii kama mtu mzima ni wakati wa kujivunia sana.” Son alisema.

 

“Nahitaji mazingira mapya ya kujipa changamoto. Nahitaji mabadiliko kidogo, miaka 10 ni muda mrefu,” Son aliongeza. “Nilitumia muda mwingi kutafakari kama nilitaka kupata uzoefu wa soka katika mazingira tofauti.”

 

Tottenham wako Seoul kama sehemu ya maandalizi yao ya kabla ya msimu mpya, Son ataanza na nahodha wa timu dhidi ya Newcastle katika mechi yao ya kirafiki siku ya Jumapili, ikimaanisha kuwa mechi yake ya mwisho katika klabu hiyo inaweza kuchenzwa nchini mwake.

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *