WAHAMIAJI WASIO NA VIBALI KUPELEKWA GUANTANAMO

WAHAMIAJI WASIO NA VIBALI KUPELEKWA GUANTANAMO

  • Habari
  • January 30, 2025
  • No Comment
  • 108

Kufuatia Amri Ya Kuwaondoa Raia Wote Wanaoishi Bila Vibali, Rais Wa Marekani, Donald Trump, Ametangaza Mipango Ya Kuandaa Kituo Cha Kuwazuia Wakimbizi Hao Katika Gereza La Kijeshi La Guantanamo.

 

Vyama Vya Wafanyakazi Wa Serikali Nchini Marekani Vimewashauri Wanachama Wake Kuwa Makini Na Utawala Wa Trump Na Kupendekeza Mpango Wa Kujitolea Kujiuzulu Mpango Ambao Utawawezesha Wafanyakazi Kujiuzulu Kwa Malipo Ya Mshahara Wa Miezi Minane.

 

Wakati Huo Rais Wa Cuba, Miguel Diaz-Canel, Ameielezea Mipango Hiyo Kuwa Ya Ukatili, Akidai Kuwa Wakimbizi Hao Watawekwa Karibu Na Vituo Vilivyotumika Kwa Mateso Na Vifungo Vinavyokiuka Sheria.

 

Kituo Hicho, Ambacho Ni Tofauti Na Gereza Hilo Lenye Ulinzi Mkali, Kiliwahi Kutumika Miaka Ya Nyuma Kuhifadhi Wakimbizi, Wakiwemo Wahaiti Na Wacuba Waliokamatwa Baharini Na Kitakua Na Uwezo Wa Kupokea Wahamiaji Elfu 30.

✍️| Kastul Elias

Related post

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…
TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *