WANAOPIGA MZIKI KUPITA KIASI WAONYWA

WANAOPIGA MZIKI KUPITA KIASI WAONYWA

Baraza la Taifa la Uhifadhi wa Mazingira NEMC limetoa onyo kwa wamiliki wa kumbi za starehe (Baa) nchini kuhakikisha wanafuata sheria za utunzaji wa mazingira.

 

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza hilo Immaculate Swale, wakati akiwasilisha taarifa ya mafanikio ya Baraza hilo katika kipindi cha miaka minne cha awamu ya sita ya utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan, ambapo amesema wataendelea kuwatafta kwa kushirikiana  na jeshi la polisi na kuwafikisha katika mamlaka husika ili wachukuliwe hatua za kinidhamu.

 

Immaculate amesema kumekuwepo na tabia ya baadhi ya wamiliki wa kumbi hizo kupiga mziki Kupitia kiasi Hali inayosababisha mtetemo mkubwa na kusababisha kero kwa Wananchi hasa wanaoishi maeneo jirani na kumbi hizo, ambapo Katika kipindi cha miaka minne (4), jumla ya kaguzi 9,606 zilifanyika na malalamiko 1,483 yalishughulikiwa hasa katika eneo la kelele na mitetemo.

 

Aidha, pia amewataka wamiliki wa vyombo vya moto, Makanisa na Misikiti kuhakikisha wanafuata kanuni na sheria za utunzaji wa mazingira ili kutokusabisha kero kwa wakazi wa karibu na maeneo hayo.

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *