DKT NATU AKUTANA NA WAKURUGENZI WA IMF JIJINI WASHINGTON

DKT NATU AKUTANA NA WAKURUGENZI WA IMF JIJINI WASHINGTON

  • Habari
  • October 14, 2025
  • No Comment
  • 12
16 / 100 SEO Score

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, DKT. Natu El-maamry Mwamba (kushoto), akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika wa Shirika la Fedha la Kimataifa( IMF) , Bw. Adran Ubisse, baada ya kikao chao kilichofanyika Makao Makuu ya Taasisi hiyo, Jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambapo katika mazungumzo yao Bw. Ubisse aliipongeza Tanzania kwa kuwa na rekodi nzuri ya utekelezaji wa miradi kwa kutumia vizuri fedha inazokopa.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, DKT. Natu El-maamry Mwamba (kushoto), akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anayesimamia Idara ya Afrika, Bw. Abebe Selassie, Makao Makuu ya Taasisi hiyo, Jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambapo pamoja na mambo mengine Bw. Abebe amemmwagia sifa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kusimamia vema sera za uchumi na fedha za nchi yake ikiwemo kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na namna anavyosimamia fedha za miradi zinazotolewa na Taasisi hiyo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikilinganishwa na nchi nyingi za Afrika.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, DKT. Natu El-maamry Mwamba (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika wa Shirika la Fedha la Kimataifa( IMF) , Bw. Adran Ubisse ( wa pili kulia), Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba (wa kwanza kulia), Katibu Mkuu-Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango-Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil (wa pili kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Dkt. Elsie Kanza (wa kwanza kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichofanyika makao makuu ya IMF, jijini Washington D.C, nchini Marekani.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, DKT. Natu El-maamry Mwamba (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anayesimamia Idara ya Afrika, Bw. Abebe Selassie (wa pili kulia), Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba (wa kwanza kulia), Katibu Mkuu-Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango-Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil (wa pili kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Dkt. Elsie Kanza (wa kwanza kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichofanyika makao makuu ya IMF, jijini Washington D.C, nchini Marekani.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Washington D.C)

Related post

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera,akizungumza…
RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA HASARA

RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA…

11 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Bw. Missaile Musa amesema mafunzo yanayotolewa…
BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *