
MALAWI YAZUIA BIDHAA ZA KILIMO ZA TANZANIA
- Habari
- April 17, 2025
- No Comment
- 14
Serikali imetangaza kuwa itazuia uingizaji wa mazao na bidhaa zote za kilimo kutoka Malawi na Afrika Kusini kufikia siku ya Jumatano ijayo, iwapo nchi hizo hazitabadilisha msimamo wao wa kuweka vikwazo dhidi ya bidhaa za kilimo kutoka Tanzania.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe na kuongeza kuwa licha ya jitihada za kidiplomasia na mawasiliano na Waziri wa Kilimo wa Malawi, bado hakuna majibu yoyote rasmi, na hivyo serikali inalazimika kuchukua hatua za kulinda maslahi ya wakulima na wafanyabiashara wa ndani.
“Ni vyema ifahamike kuwa kwa kipindi cha miaka mitano, Serikali ya Tanzania imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kufungua soko la ndizi nchini Afrika Kusini bila mafanikio. Hali hii inafanana na changamoto tulizopitia kwa zaidi ya miaka kumi katika kufungua soko la parachichi, hadi pale tulipoamua kuchukua hatua za kulinda maslahi ya nchi yetu,”
Hatua hiyo inafuatia taarifa rasmi kuwa Serikali ya Malawi imezuia uingizwaji wa bidhaa kadhaa za kilimo kutoka Tanzania, ikiwemo unga, mchele, tangawizi, ndizi na mahindi, hatua iliyosababisha usumbufu mkubwa kwa wafanyabiashara wa Tanzania wanaosafirisha bidhaa hizo.