NEMC IPO VIWANJA VYA NANENANE DODOMA- MAONESHO YA WAKULIMA

NEMC IPO VIWANJA VYA NANENANE DODOMA- MAONESHO YA WAKULIMA

  • Habari
  • August 1, 2025
  • No Comment
  • 48
13 / 100 SEO Score
Na.Mwandishi Wetu.
BARAZA  la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma, likitoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda na kuhifadhi mazingira kupitia kilimo rafiki kwa mazingira.
Kupitia banda lake, NEMC inatoa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya mazingira, ikiwa ni pamoja na umuhimu wa kufanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) kabla ya kuanzisha miradi ya kilimo, ujenzi na shughuli nyingine za kiuchumi.

Aidha, elimu nyingine inayotolewa ni kuhusu,Katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki,Athari za uchafuzi wa vyanzo vya maji,Umuhimu wa kuzingatia kilimo hifadhi,Ulipaji wa ada za mazingira kwa mujibu wa sheria na Elimu ya urejelezaji wa taka kwa ajili ya kulinda mazingira na kuongeza kipato.

Maonesho ya Nanenane mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.” NEMC imesisitiza kuwa uchaguzi wa viongozi wenye maono katika sekta hizo ni msingi wa utekelezaji wa sera na sheria za mazingira kwa maendeleo endelevu.

Baraza hilo limewahimiza wakulima, wafugaji, wavuvi na wananchi wote wanaotembelea maonesho hayo kutembelea banda la NEMC ili kupata elimu sahihi juu ya mbinu bora za kilimo na uzalishaji zinazozingatia utunzaji wa mazingira.

“Ustawi wa kilimo na uchumi wetu unategemea sana afya ya mazingira yetu. Tunawahamasisha wananchi kufika kujifunza na kushirikiana nasi katika kulinda mazingira kwa kizazi cha sasa na kijacho,” imesema NEMC.

Maonesho ya Nanenane kitaifa yameanza rasmi Agosti 1 na yanatarajiwa kufikia kilele chake Agosti 8, 2025.

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *