TLS YALAANI VITENDO VYA UDHALILISHAJI DHIDI YA LISSU

TLS YALAANI VITENDO VYA UDHALILISHAJI DHIDI YA LISSU

  • Habari
  • August 1, 2025
  • No Comment
  • 34
11 / 100 SEO Score

Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) kimelaani vitendo wanavyodai ni udhalilishaji na ukandamizaji vinavyofanywa na Jeshi la Magereza dhidi ya Mwanachama wao, Wakili Tundu Lissu wakati shauri lake likiendelea Mahakamani.

TLS imesema vitendo anavyofanyiwa vinakiuka Katiba ya Tanzania na Mikataba ya Kimataifa inayolinda haki, na utu wa kila Mtu.

 

TLS imeomba kukutana na Jaji Mkuu kujadili suala hilo na kulitaka Jeshi la Magereza kuacha mara moja vitendo hivyo, ikiwemo kuzuia askari wasiotambulika kuingia mahakamani na kuwachukulia hatua askari wote waliohusika katika shambulio dhidi ya Lissu, Julai 30, 2025.

 

Chama hicho kimesema iwapo mambo haya hayataheshimiwa, Uongozi wa TLS hautasita kuchukua hatua za dharura kulinda hadhi za Wanachama wake na Haki Jinai Nchini ili kutuma ujumbe wa wazi na thabiti dhidi ya ukiukwaji wa haki za Wakili yeyote.

Credit: Jamii Forums

 

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *