WAZIRI NDEJEMBI AAGIZA UKUTA KUBOMOLEWA KIGOGO

WAZIRI NDEJEMBI AAGIZA UKUTA KUBOMOLEWA KIGOGO

  • Habari
  • February 15, 2025
  • No Comment
  • 77

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Deogratius Ndejembi, ametoa siku mbili kuanzia leo Februari 15, 2025, kwa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuvunja sehemu ya ukuta wa kiwanja namba P18618 kilichopo Kigogo, Dar es Salaam, baada ya mmiliki wake kushindwa kuwasilisha nyaraka za umiliki halali.

 

Waziri Ndejembi amesisitiza kuwa uchunguzi wa wataalamu kupitia Kamishna wa Ardhi ulibaini kuwa Kampuni ya Nizar Food ilijiongezea ukubwa wa eneo lake kinyume cha sheria na kulijengea ukuta na hivyo sehemu ya ukuta huo unapaswa kubomolewa ili kulinda maeneo ya wazi.

 

Ikumbukwe kuwa, januari 21 mwaka huu Waziri Ndejembi alifika katika eneo hilo lenye mgogoro wa muda mrefu kati ya wananchi na mmiliki wa kiwanja hicho kampuni ya Nizar Food ambapo aliwataka wamiliki hao kuwasilisha nyaraka zinazoonesha uhalali wa kuongeza ukubwa wa kiwanja hicho, lakini hawakufanya hivyo ndani ya muda aliotoa.

✍️| Kastul Elias

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *