
TIMU YA TAIFA YA NGUMI YAENDELEA NA MAZOEZI MAZITO
- Habari
- February 23, 2025
- No Comment
- 49
Timu ya Taifa ya ngumi kwa upande wa wanawake imeeendelea na mazoezi katika kambi iliyopo Mbezi Beach Dar es Salaam kwaajili ya kujiandaa na mashindano ya ubingwa wa Dunia nchini Serbia mwezi machi mwaka huu.
Kambi hiyo ya siku 20 kwaajili ya maandalizi ya mabondia hao itavunjika rasmi machi tatu na siku inayofuata baada ya hapo itakua ni kwaajili ya safari ya kuelekea nchini Serbia kwaajili ya kushiriki mashindano hayo makubwa duniani.
Jumla ya dola za kimarekani 2.88 milioni zimeandaliwa kama zawadi kwa washindi wa mashindano hayo ambapo mshindi wa medali ya dhahabu atajizolea dola za kimarekani 100, 000 huku mshindi wa medali ya fedha akijizolea ni dola za kimarekani 50,000.
Medali ya shaba mshindi atajizolea kitita cha dola za kimarekani 25,000 na washindi wa tano bora watajizolea dola za kimarekani 10,000.
✍️| @kastulelias_