RAILA ODINGA AFARIKI DUNIA

RAILA ODINGA AFARIKI DUNIA

  • Habari
  • October 15, 2025
  • No Comment
  • 7
9 / 100 SEO Score

WAZIRI Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga, amefariki dunia leo Jumatano 15,2025 akiwa na umri wa miaka 80.

Taarifa zinaeleza kuwa kiongozi huyo wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM)amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali moja nchini India.

Kifo chake kimetokea wiki chache baada ya kuzagaa tetesi mitandaoni zilizodai kuwa alikuwa katika hali mahututi, madai ambayo familia yake ilikuwa imekanusha vikali.

Awali, kaka yake mkubwa ambaye pia ni Seneta wa Siaya, Dkt. Oburu Odinga, aliwahakikishia Wakenya kuwa Raila alikuwa anaendelea kuimarika kiafya na alikuwa akipata nafuu nchini India.

Akizungumza na vyombo vya habari, Dkt. Oburu alikanusha taarifa zilizodai kwamba Raila alikuwa katika hali mbaya, akizitaja kuwa zimezidishwa na hazikuwa sahihi.

Related post

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…
TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *