WAZIRI DKT STERGOMENA TAX AZUNGUMZA NA BODABODA MAGU

WAZIRI DKT STERGOMENA TAX AZUNGUMZA NA BODABODA MAGU

  • Habari
  • September 21, 2025
  • No Comment
  • 23
13 / 100 SEO Score

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax, tarehe 20 Septemba 2025, alikutana na kufanya Kikao na Viongozi wa Maafisa usafirishaji kwa njia ya Pikipiki (Bodaboda) wakiwawakilisha kundi kubwa la Bodaboda Wilaya Magu mkoani Mwaanza, Kikao ambacho kimetokana na maombi ya mara kwa mara ya Viongozi wa Bodaboda kuomba miadi ya kukukutana na kuzungumza na Waziri Dkt. Tax. Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Wilaya Magu ndugu Fratha Andrea Katumwa.

Baada ya kusikiliza changamoto za Maafisa usafirishaji hao, Dkt Tax amewapongeza kwa umoja wao na kuahidi kushirikiana na Uongozi wa Wilaya Magu kuzitatua changamoto hizo haraka iwezekanavyo ili kuwapunguzia adha hizo ikiwemo uanzishwaji wa SACOS ya Bodaboda Magu.

Aidha, ametoa wito kwa Viongozi hao kuwahamasisha wafuasi wao kujitokeza kwenda kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu tarehe 29 Oktoba 2025 ili kutumia haki yao ya Kikatiba.

Akihitimisha, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, amewataka Bodaboda kote nchini kuwa mabalozi wazuri wa kulinda amani ya Nchi wawapo katika shughuli zao kwakuwa wanakutana na kuwahudumia watu wengi hivyo watumie fursa vilivyo na wajiepushe na vitendo vya uhalifu ili waweze kujiletea maendeleo.

Related post

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

WAFANYABIASHARA, WAJASIRIAMALI HANDENI WAFUNGUKA SABABU ZA KUJITOKEZA KUPIGA KURA…

18 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score   Na Augusta Njoji, Handeni TC Makundi mbalimbali ya wananchi katika…
REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *