MTAALAMU WA LISHE HANDENI AFICHUA SIRI YA MAKUNDI SITA YA CHAKULA BORA

MTAALAMU WA LISHE HANDENI AFICHUA SIRI YA MAKUNDI SITA YA CHAKULA BORA

  • Habari
  • October 15, 2025
  • No Comment
  • 12
13 / 100 SEO Score

HANDENI-TC

Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Handeni, mkoani Tanga, Esther Herman, ametoa wito kwa wananchi kuzingatia ulaji wa chakula bora kinachojumuisha makundi sita muhimu ili kuepuka magonjwa yatokanayo na lishe duni.

Akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Chakula Duniani yanayofanyika kitaifa jijini Tanga, chini ya kaulimbiu “Tuungane pamoja kupata chakula bora kwa maisha bora ya baadaye”, Esther ametaja makundi hayo ni wanga, protini, mboga za majani, matunda, mafuta pamoja na maji.

Amesema kila kundi lina umuhimu wake mwilini, na ulaji usio sahihi unaweza kusababisha udhaifu wa kinga ya mwili, utapiamlo, au uzito uliopitiliza.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa elimu ya lishe kuanzia ngazi ya kaya, akibainisha kuwa jamii nyingi bado hazina uelewa sahihi kuhusu mlo kamili, jambo linalochangia changamoto za afya kwa watoto na watu wazima.

Related post

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

SERIKALI YAPANGA KUIMARISHA UBORA NA USALAMA WA  CHAKULA

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera,akizungumza…
RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA HASARA

RAS ARUSHA: MAFUNZO YA PPRA YATAONDOA UWEZEKANO WA KUPATA…

11 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Bw. Missaile Musa amesema mafunzo yanayotolewa…
BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

BIL 527 ZATEKELEZA MIRADI 13 YA TANROADS TABORA-ENG MLIMAJI

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *