HANDENI MJI YAFANYA BONANZA LA MICHEZO KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

HANDENI MJI YAFANYA BONANZA LA MICHEZO KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29

  • Habari
  • October 19, 2025
  • No Comment
  • 6
15 / 100 SEO Score

HANDENI TC

Halmashauri ya Mji wa Handeni imefanya bonanza kubwa la michezo lililolenga kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Bonanza hilo limefanyika leo katika Uwanja wa Kigoda, Handeni, na limehusisha wananchi, watumishi wa umma, viongozi wa dini, viongozi wa kisiasa na taasisi binafsi.

Akizungumza katika bonanza hilo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewataka wananchi wote waliojiandikisha kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kupiga kura ili kutimiza haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka.

“Nawasihi wananchi wote wa Handeni kujitokeza mapema siku ya uchaguzi. Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa saa 1:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni. Serikali imeimarisha ulinzi na usalama, hivyo kila mmoja atapiga kura kwa amani na utulivu kama tulivyoshiriki bonanza letu leo,” amesema Mhe. Nyamwese.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Handeni, Maryam Ukwaju, amewahimiza watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla kuendeleza ushirikiano na mshikamano kupitia michezo, akibainisha kuwa michezo ni chachu ya umoja na afya bora.

Bonanza hilo lilihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, kukimbia, kuvuta kamba, na mbio za taratibu.

Related post

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

REA YAANZA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MKOANI MARA

14 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza mitungi ya gesi 19,530…
SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI*.

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano,…
TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

TANZANIA YAJIPANGA KUONGOZA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA COP30

16 / 100 Powered by Rank Math SEO SEO Score Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *